UKOO WA NDOSI.

– Ukoo wa Ndosi ni ukoo mkongwe sana na unaopatikana kwa wingi sana katika kijiji cha Mbweera, Masama kati. Ukoo wa Ndosi ni tawi la ukoo wa Mboro ambao tulishaujadili hapa kwa kina na matawi yake lakini tawi lilikuwa na nguvu sana katika eneo hili la Masama kati na ndio ulikuwa ukoo wa watawala eneo …

UKOO WA NG’UNDA.

– Ukoo wa Ng’unda ni ukoo wa wachagga unaopatikana katika vijiji vya Masama Magharibi kama vile Ng’uni. Huu ni ukoo ambao sio mkubwa sana lakini una watu wengi makini unaoweza kukutana nao katika maeneo mbalimbali. – Hakuna taarifa za kutosha sana kujua chanzo chake halisi au kama huenda ni tawi la ukoo mwingine mkubwa zaidi …

UKOO WA MOSI.

– Ukoo wa Mosi ni ukoo unaopatikana katika himaya ya umangi Siha/Sanya Juu. Hakuna taarifa nyingi juu ya chimbuko la ukoo huu wala uelewa zaidi kama laba ni tawi la ukoo mwingine mkubwa unaojulikana zaidi. – Hata hivyo ukoo wa Mosi ni ukoo wa watu makini na wapambanaji pia. Tumekutana na watu kadhaa wenye uwezo …

UKOO WA KIRUNDWA.

– Ukoo wa Kirundwa au wakati mwingine huitwa Kihundwa ni ukoo mdogo unaopatikana kwa wingi zaidi katika kijiji cha Mese, Siha/Sanya Juu. Ukoo wa Kirundwa unapatikana pia kwa uchache katika vijiji vingine vya Siha/Sanya Juu. – Kwa mujibu wa taarifa zisizo rasmi inasemekana kwamba ukoo wa Kirundwa huenda ni tawi la ukoo wa Munuo wenye …

UKOO WA MASAKI.

– Ukoo wa Masaki ni ukoo maarufu katika eneo la himaya ya umangi Siha/Sanya Juu katika vijiji vya Samaki Maini na Mae. Wachagga wa ukoo wa Masaki wakiwa wameshuka kutoka kwenye plango ya Shira waliweka makazi yao ya mwanzoni ya kudumu katika kijiji cha Samaki Maini sambamba na ukoo wa Orio/Urio na Kileo. – Kutoka …

UKOO WA MWANDRI.

– Ukoo wa Mwandri ni ukoo mkongwe sana na maarufu katika eneo la Siha Sanya Juu. Huu ni ukoo ambao uliweka makazi yake ya kudumu katika kijiji cha Wanri, Siha upande wa juu wa hospitali ya Kibong’oto. Kijji hiki cha Wanri miaka ya baadaye kilikuja kuwa maarufu zaidi na muhimu zaidi kwenye masuala ya utawala …

UKOO WA NATAI

– Ukoo wa Natai ni ukoo mkongwe pia na mashuhuri sana upande wa Magharibi ya Kilimanjaro. Huu ni ukoo ambao unapatikana kwa wingi zaidi katika eneo la Masama magharibi katika vijiji vya Lukani, Mashua, Nkwansira, Ng’uni, Kyuu, Losaa n.k. Ukoo wa Natai wanapatikana kwa wingi pia katika vijiji vya himaya ya umangi Sanya Juu. – …

UKOO WA MUNUO.

– Ukoo wa Munuo ni ukoo mkubwa na mashuhuri sana upande wa magharibi ya mbali ya Uchaggani Kilimanjaro. Ukoo huu unapatikana katika maeneo ya Masama Magharibi hususan katika vijiji vya Lukani, Ng’uni, Kyuu, Mashua, Nkwansira, Losaa n.k. Ukoo huu unapatikana pia kwa kiasi maeneo ya Sanya Juu. – Kutoka kwenye historia ukoo wa Munuo unafahamika …

UKOO WA NKINI.

– Ukoo wa Nkini ni moja kati ya koo kongwe kabisa na mashuhuri sana katika eneo la Siha/Sanya Juu. Ukoo wa Nkini sambamba na koo nyingine katika eneo hilo walishuka kutoka kwenye plango ya Shira(Shira Plateau) na kuweka makazi yao katika vijiji vya ukanda wa juu wa himaya ya umangi Siha/Sanya Juu hususan kijiji cha …

UKOO WA MMARI.

UKOO WA MMARI. – Ukoo wa Mmari ukoo mkubwa wenye historia kubwa na uliotoa watu mashuhuri katika historia ya wachagga. Kutoka kwenye historia ukoo wa Mmari huenda chimbuko lake kwa uchaggani ni Siha/Sanya ambapo wanapatikana kwa wingi sana na umewahi kuwa ukoo wenye nguvu na uliotoa watawala imara sana wa himaya ya umangi Siha/Sanya Juu. …