HADITHI YA WACHAGGA INAYOONYESHA MADHARA YA MTU KUKOSA SHUKRANI KWA “RUWA”.

Hapo zamani za kale katika nchi ya wachagga kulikuwa na mwanamke ambaye hakujaliwa kabisa kupata mtoto hata mmoja. Mwanamke huyu pia umri wake wa kuweza kupata mtoto ulikuwa umepita sana. Kila siku alikuwa akifanya kazi mpaka kufikia kuchoka sana huku wanawake wengine wakimkejeli na kumsanifu kwa kutokuwa na mtoto ambaye angeweza kuwa msaada kwake. Jambo …

HADITHI YA “MORILE” KWA WACHAGGA.

Hapo zamani za kale wachagga walifahamu kwamba kulikuwa na Mungu aliyeumba watu ambaye aliishi kwenye juu huko juu mawinguni. Wachagga walijua pia kwamba Mungu huyo amewatendea watu mambo mema mengi sana. Lakini wachagga waliendelea kuliangalia anga la juu na kutamani kufahamu mambo mengi sana kuhusu anga ambalo jua hupita kila siku. Lakini hawakuweza kupata mtu …

HADITHI ZA DINI YA ASILI YA WACHAGGA KABLA YA KUJA KWA WAMISIONARI WA KIKRISTO – 3

RUWA/IRUWA AINGAMIZA DUNIA. Hapo zamani za kale watu waliendekeza uvivu na kutelekeza majukumu yao na kuwaagiza watu maskini na wanyonge kuwafanyia kazi zao. Kisha watu matajiri wakagoma kabisa kufanya kazi kwa namna yoyote ile. Walisubiri mpaka watu maskini na wenye uhitaji kuvuna mazao yao na mara baada ya kuvuna matajiri na wenye uwezo waliwapora kwa …

HADITHI ZA DINI YA ASILI YA WACHAGGA KABLA YA KUJA KWA WAMISIONARI WA KIKRISTO – 2

Baada ya Ruwa/Iruwa kupotea na kutoonekana tena kiongozi mkuu wa wachagga aliamua kusali kwa kumwomba Ruwa/Iruwa kwa ajili ya asali na maziwa. Ruwa/Iruwa alisikia sala hiyo na kumtuma tena waziri wake msaidizi kwa kiongozi mkuu wa wachagga. Ruwa/Iruwa alimtuma waziri akamwaambie kiongozi mkuu wa wachagga, “Sasa nimeamua kuwaonea huruma wewe na watu wako. Kuanzia sasa …