UKOO WA NDOSSA.

– Ukoo wa Ndossa ni ukoo wa Wachagga wanaopatikana upande wa magharibi ya Kilimanjaro. Huu ni ukoo mkubwa kiasi Machame ya magharibi na mashariki ukiwa na ngome yake katika kijiji cha Saawe, Masama. – Watu wengi wamekuwa wakiamini kwamba kuna uwezekano wa kuwepo kwa uhusiano kati ya ukoo huu wa Ndossa na ukoo wa Ndosi …

UKOO WA SIAO.

– Ukoo wa Siao ni ukoo wa Wachagga wanaopatikana upande wa magharibi ya Kilimanjaro. Huu ni ukoo ambao sio maarufu sana lakini unapatikana kwa kiasi kwenye baadhi ya vijiji. – Wachagga wa ukoo wa Siao wanapatikana Masama magharibi katika kijiji cha Lukani na vijiji jirani. Hakuna taarifa nyingi zinazopatikana juu ya makazi ya asili Uchaggani …

UKOO WA MWASHA

– Ukoo wa Mwasha ni ukoo maarufu na mkongwe sana uchaggani hususan katika upande wa magharibi ya Kilimanjaro. Wachagga wa ukoo wa Mwasha ambao wanapatikana kwa wingi zaidi katika kijiji cha Mudio, Masama au Machame ya magharibi kwa ujumla ni watu makini na wenye kujituma sana katika maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi wanakopatikana. …

UKOO WA NDOSI.

– Ukoo wa Ndosi ni ukoo mkongwe sana na unaopatikana kwa wingi sana katika kijiji cha Mbweera, Masama kati. Ukoo wa Ndosi ni tawi la ukoo wa Mboro ambao tulishaujadili hapa kwa kina na matawi yake lakini tawi lilikuwa na nguvu sana katika eneo hili la Masama kati na ndio ulikuwa ukoo wa watawala eneo …

UKOO WA NG’UNDA.

– Ukoo wa Ng’unda ni ukoo wa wachagga unaopatikana katika vijiji vya Masama Magharibi kama vile Ng’uni. Huu ni ukoo ambao sio mkubwa sana lakini una watu wengi makini unaoweza kukutana nao katika maeneo mbalimbali. – Hakuna taarifa za kutosha sana kujua chanzo chake halisi au kama huenda ni tawi la ukoo mwingine mkubwa zaidi …

UKOO WA MOSI.

– Ukoo wa Mosi ni ukoo unaopatikana katika himaya ya umangi Siha/Sanya Juu. Hakuna taarifa nyingi juu ya chimbuko la ukoo huu wala uelewa zaidi kama laba ni tawi la ukoo mwingine mkubwa unaojulikana zaidi. – Hata hivyo ukoo wa Mosi ni ukoo wa watu makini na wapambanaji pia. Tumekutana na watu kadhaa wenye uwezo …

UKOO WA KIRUNDWA.

– Ukoo wa Kirundwa au wakati mwingine huitwa Kihundwa ni ukoo mdogo unaopatikana kwa wingi zaidi katika kijiji cha Mese, Siha/Sanya Juu. Ukoo wa Kirundwa unapatikana pia kwa uchache katika vijiji vingine vya Siha/Sanya Juu. – Kwa mujibu wa taarifa zisizo rasmi inasemekana kwamba ukoo wa Kirundwa huenda ni tawi la ukoo wa Munuo wenye …

UKOO WA MASAKI.

– Ukoo wa Masaki ni ukoo maarufu katika eneo la himaya ya umangi Siha/Sanya Juu katika vijiji vya Samaki Maini na Mae. Wachagga wa ukoo wa Masaki wakiwa wameshuka kutoka kwenye plango ya Shira waliweka makazi yao ya mwanzoni ya kudumu katika kijiji cha Samaki Maini sambamba na ukoo wa Orio/Urio na Kileo. – Kutoka …

UKOO WA MWANDRI.

– Ukoo wa Mwandri ni ukoo mkongwe sana na maarufu katika eneo la Siha Sanya Juu. Huu ni ukoo ambao uliweka makazi yake ya kudumu katika kijiji cha Wanri, Siha upande wa juu wa hospitali ya Kibong’oto. Kijji hiki cha Wanri miaka ya baadaye kilikuja kuwa maarufu zaidi na muhimu zaidi kwenye masuala ya utawala …

UKOO WA NATAI

– Ukoo wa Natai ni ukoo mkongwe pia na mashuhuri sana upande wa Magharibi ya Kilimanjaro. Huu ni ukoo ambao unapatikana kwa wingi zaidi katika eneo la Masama magharibi katika vijiji vya Lukani, Mashua, Nkwansira, Ng’uni, Kyuu, Losaa n.k. Ukoo wa Natai wanapatikana kwa wingi pia katika vijiji vya himaya ya umangi Sanya Juu. – …